Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Taarifa za kuwepo mtu mwenye dalili za Ebola Tanzania

MTU mmoja ambaye ni mkimbizi kutoka Burundi, amefariki dunia baada ya kuugua ugonjwa wenye dalili zinazofanana na Ugonjwa wa Ebola katika Kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma.

Marehemu huyo aliyejulikana kwa jina la Buchimu Joel, alifariki dunia jana Agosti 10, 2015 katika Hospitali ya Mkoa wa Kigoma ya Maweni, baada ya kuugua kwa siku kadhaa akiwa katika Kambi hiyo.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Shija Ganai, amekaririwa na FikraPevu akisema kwamba mtu huyo alikuwa akitokwa na damu katika sehemu zote za matundu za mwili wake na kwamba sampuli za damu na vitu vingine zimepelekwa Jijini Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi.

Aidha, amebainisha kwamba kutokana na dalili hizo ambazo zinafanana na za ugonjwa wa Ebola, wataalamu wa afya walimhudumia kwa kufuata misingi ya kutibu magonjwa ya Ebola ambapo wamelazimika kumzika kwa kufuata taratibu pamoja na kuweka tahadhari katika Karantini ya maeneo aliyokaa akiwa mgonjwa pamoja na ndugu wa karibu.
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba, homa ya Ebola ilianza nchini Guinea na kutapakaa nchi jirani za Sierra Leone na Liberia mwaka jana huku ikielezwa kuua watu wengi ambao idadi yao hadi sasa inadaiwa kuzidi watu 10,000 baada ya kuibuka kwa tishio la ugonjwa huo katika siku za karibuni katika mataifa mbalimbali mapema mwaka huu.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, dalili za awali za ugonjwa huo ni homa kali ya ghafla, kulegea mwili, maumivu ya misuli, kuumwa na kichwa, na kutokwa na vidonda kooni.

Mara nyingi dalili hizo hufuatiwa na kutapika, kuharisha, kutokwa na vipele vya ngozi, figo na ini kushindwa kufanya kazi na kwa baadhi ya wagonjwa, hutokwa damu ndani na nje ya mwili.

Serikali ilisema katika mkoa wa Dar es Salaam, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Temeke Isolation Unit, zilitengwa maalum kwa kuhudumia wagonjwa wa ebola endapo watatambuliwa ambapo eneo la Temeke linaelezwa kuwa limeboreshwa kwa kuzingatia vigezo maalumu ili likidhi mahitaji ya matibabu ya ugonjwa huu.
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

www.7x24hours.blogspot.com
© Copyright 24hours
Back To Top