Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Lulu avamiwa

LULU547.jpg 
BAD news! Mtoto mzuri Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amekumbwa na masaibu mapya ya kuvamiwa na vibaka nyumbani kwake, Mbezi Beach jijini Dar na kumuibia simu zake mbili aina ya Iphone.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni ambapo wezi hao wanadaiwa kuruka ukuta na kufanikiwa kuvunja dirisha la chumba anacholala mrembo huyo na kumliza simu hizo huku yeye akiwa amelala fofofo.
Kwa mujibu wa chanzo makini, wezi hao walitumia mbinu za ‘kisayansi’ kutekeleza zoezi lao kwani siku hiyo Lulu alirudi nyumbani mapema na akawa anachati kwa kutumia moja ya simu hizo, ghafla akapitiwa ambapo alikuja kushtuka na kukuta dirisha limevunjwa na simu zimetoweka.
“Nimemhurumia sana Lulu kwa kuwa siku ambayo ameibiwa, simu kesho yake tena akafiwa na bibi yake mzaa mama ambaye ndiye alikuwa kipenzi chake sana. Hapo utagundua alipata majanga kiasi gani maana wakati alikuwa bado anafikiria ishu ya simu huku tena akakumbana na janga la kifo.
“Amelazimika kutafuta simu nyingine anayoitumia sasa tofauti na awali alikuwa nazo mbili,” kilisema chanzo hicho.
Paparazi wetu baada ya kupenyezewa ubuyu huo, alimtafuta Lulu ili aizungumzie ishu hiyo, ambapo alikiri kufikwa na masaibu hayo huku akishindwa kufafanua zaidi juu ya tukio hilo kwa kile alichodai alikuwa sehemu yenye kelele.
“Ni kweli nimepata matatizo sana mwezi huu ikiwa pamoja na hilo la kuibiwa simu, sema kwa hapa nilipo siwezi kuzungumzia lolote maana nipo katikati ya watu wengi na kuna makelele sana. Lakini itakuwa vyema nikikutafuta baadaye,” alisema.
Licha ya Lulu kutotaja kiasi, simu hizo zinakadiriwa kufikia kiasi cha shilingi milioni tatu.
 
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

www.7x24hours.blogspot.com
© Copyright 24hours
Back To Top