Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

JOKATE AFANYA VURUGU KUBWA USIKU NYUMBANI KWAO OYSTERBAY

 Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
Staa mwenye jina kubwa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ anadaiwa kufanya vurugu nyumbani kwao usiku baada ya kutwaa Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike 2015 katika tuzo zilizotolewa na waandaaji wa Tamasha la Kimataifa la Filamu (ZIFF) hivi karibuni visiwani Zanzibar.
Habari kutoka kwa chanzo chetu ambacho ni mtu wa karibu
wa staa huyo wa sinema na Bongo Fleva zilieleza kuwa, awali Jokate ambaye hakwenda Zanzibar, hakujua chochote kuhusiana na tuzo hizo hivyo alipopewa taarifa na mtu ambaye alikuwepo kwenye tamasha hilo, alishindwa kujizua na kuanza kutimua mbio ovyo huku viatu akiwa ameviacha katika mgahawa aliokuwa amekaa jirani na nyumbani kwao, Oysterbay jijini Dar.
“Unajua Jojo (Jokate) alikuwa hajui kuhusiana na tuzo hiyo, alikuwa amekaa kwenye mgahawa mishale ya saa 3:00 usiku, jirani na nyumbani kwao.
“Alipoambiwa ameshindwa ndiyo akakimbilia nyumbani na kuanza kubamiza mageti na kutupatupa vitu, jambo lililosababisha taharuki nyumbani hapo na kusababisha wazazi wake kuhofu wakijua labla mtoto wao amepata kichaa,” kilisema chanzo hicho.
Kilisema kwamba, baada ya kuulizwa kulikoni kupagawa kiasi hicho ndipo akafunguka kuwa siyo kwamba alichanganyikiwa bali ilikuwa ni furaha ya kutwaa tuzo hiyo.
Gazeti hili lilipomtafuta Jokate alikiri kutokea kwa hali hiyo na kusema kuwa alipata mshtuko mkubwa na furaha kwa kuwa hakutegemea jambo kama hilo.
“Ukifanya kitu watu wakakukubali ni furaha kubwa na unapata moyo wa kufanya zaidi na zaidi,” alisema Jokate.
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

www.7x24hours.blogspot.com
© Copyright 24hours
Back To Top