Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Wakazi Wa Mgao Wamvaa Halima Mdee Kwa Kuwadhalilisha......Wamtaka Afute Kauli Yake


KUFUATIA taarifa iliyotolewa  na Waziri Kivuli, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halima Mdee kuhusu utoaji wa ardhi kwa bilionea Alhaji Aliko Dangote, wakazi wa kijiji cha Mgao, Halmashauri ya Mtwara Vijijini wamemtaka kufuta kauli yake.

Wakitoa malalamiko yao kwa vyombo vya habari, baadhi ya wakazi wa kijiji hicho ambao walijitambulisha kwa majina ya Seif Said na Mohamed Njiti, walisema kuwa kitendo cha ardhi yao kulinganishwa na kaniki na kipande cha kanga kimewasikitisha.

Walisema uthamini wa ardhi umeshaanza, wanatarajia kulipwa Sh milioni 10 kwa ekari moja, huku wakipata malipo ya mimea iliyopo kwenye mashamba yao, zoezi ambalo bado linaendelea katika maeneo ya vijiji vya Kisiwa na Mgao.

Kwa upade wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Abdulahman Shaha, alisema amesikitishwa na taarifa iliyotolewa kwa kulinganisha ardhi yao na kipande cha kaniki.

“Ile kauli sio sahihi, ilibidi aje Mgao apate taarifa sahihi ili akatoe bungeni, sisi tuko katika tathmini ya ardhi, kila mwananchi atalipwa stahiki yake,  walipaji wa ardhi hii ni Mamlaka ya Bandari Tanzania siyo Dangote,”  alisema Shaha. 

Naye Meneja wa Mamlaka ya Bandari Mkoa wa Mtwara, Hebel Mwasenga, alisema mamlaka hiyo inamiliki eneo la hekta 1,000, ambapo mwekezaji huyo amepewa eneo la hekta 25 kwa ajili ya ujenzi wa bandari ndogo.
Na Mpekuzi blog
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

www.7x24hours.blogspot.com
© Copyright 24hours
Back To Top