Baadhi
ya Waandishi wa habari wakifanya kazi yao na kuelekezwa namna (Cath
Lab) mtambo wa kufanya uchunguzi na kuzibua mishipa ya damu inayopeleka
damu kwenye moyo na pia kuziba matundu ndani ya moyo bila kufungua
kifua.
Katikati
ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt.
Hussein Kidanto akizungumza na waandishi wa habari. Kushoto ni Prof.
Jameel Alata ambaye ni Daktari Mwelekezi wa Magonjwa ya Watoto ambaye
ameongoza timu ya madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Prince Sultan
Cardiac Centre iliyoko Riyadhi nchini Saudi Arabia ambao watakuwepo
Muhimbili kwa siku tisa kuanzia tarehe 8 hadi 16 Mei, mwaka huu. Kulia
ni Sheikh Said Ahmed Abri ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika
lisilo la Kiserikali la Kiislam la hapa nchini liitwayo Dhi Nureyn
Islamic Foundation na shirika hili ndilo lililoratibu timu hii ya
madaktari kuja kutoa huduma.
Baadhi
ya madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Prince Sultan Cardiac Centre
iliyoko Riyadhi nchini Saudi Arabia wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi
Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakati akiwakaribisha na
kuzungumza na vyombo vya habari, leo Jijini Dar Es Salaam.
Mwezi Mei tarehe 9, mwaka 2015, Tanzania imeandika historia nyingine
baada ya kufanya Tiba ya moyo bila ya kufanya upasuaji kwa kuziba
matundu yaliyoko kwenye moyo kwa kutumia “kifaa maalum” bila kufungua
kifua kama ilivyozoeleka.
Tiba hii inafanyika kwa mara ya kwanza nchini kupitia Idara ya Tiba
na Upasuaji Moyo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili ikishirikiana na
madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Prince Sultan Cardiac Centre
iliyoko Riyadhi nchini Saudi Arabia ambao watakuwepo Muhimbili kwa siku
tisa kuanzia tarehe 9 hadi 16 Mei, mwaka huu.
Madaktari hawa wamekuja kupitia taasisi ya Al Mutanda Islami Trust ya
Uingereza. Akizungumza na wanahabari, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Hussein Kidanto amesema jumla ya
wagonjwa zaidi ya 20 wanatarajiwa kupatiwa tiba hii.
CHANZO: MICHUZI
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;
Filed Under:
Updates
on Saturday, 9 May 2015
Post a Comment